London, England. Mshambuliaji wa Arsenal, Mesut Ozil sasa ni rasmi ataendelea kubaki klabuni hapo, baada ya kukubaliana na uongzo wa klabu hiyo kumuongezea mshahara mara ya mbili ya aliokuwa akipokea awali.
Kwa mujibu wa gazeti la The Sun, mchezaji huyo atakuwa akipokea mshahara wa Pauni 280,000 kwa wiki ikiwa ni ongezeko la asilimia mia moja ya mshahara wake.
Awali, mchezaji huyo alikuwa akipokea Pauni 140,000 milioni kwa wiki. Mkataba wa mchezaji huyo ulikuwa umebaki miezi 12 kumalizika hivyo kufanya hivyo ilikuwa ni mojawapo ya mkakati wa klabu hiyo kujiimarisha kwa ajili ya msimu ujao.
0 comments :
Post a Comment