VAN GALL NDIE ALIENIANGUSHIA JUMBA BOVU UBINGWA MWAKA HUU HAKUNA-MOURINHO
KOCHA wa Manchester United, Jose Mourinho amekiri kuwa itakuwa ngumu kwa kikodsi chake kutwaa ubingwa kutokana na ubovu wa timu aliyoachiwa na Louis Van Gaal. Manchester United ilifungana bao 1-1 na Westham katika mechi ya Ligi Kuu England mwishoni mwa wiki iliyopita. United haijatwaa ubingwa tangu msimu wa 2012/13 wakati Sir Alex Ferguson alipoachia ngazi kuinoa timu hiyo. Timu hiyo imepita katika kipindi kigumu baada ya kuwa chini ya David Moyes na Van Gaal. Mourinho anakiri kuwa ana kibarua kizito kubadili kikosi kilichoachwa na Van Gaal.
0 comments :
Post a Comment