Huo unakuwa mchezo wa 34 kwa Samatta tangu amejiunga na Genk Januari mwaka huu kutoka TP Mazembe ya DRC, 18 msimu uliopita na 14 msimu huu, akifunga mabao nane, matatu msimu huu na matano msimu uliopita.
Katika mechi hizo, ni 17 tu ndiyo alianza, 10 msimu uliopita na tano msimu huu, wakati 16 alitokea benchi nane msimu uliopita na 13 msimu huu – na mechi 10 hakumaliza akitolewa, sita msimu uliopita na nne msimu huu.
Kikosi cha KRC Genk jana kilikuwa: Bizot, Castagne, Brabec, Colley, Nastic, Ndidi, Pozuelo, Susic/Heynen dk77, Bailey, Buffalo/Trossard dk89 na Karelis/Samatta dk85.
Rapid Viena: Novota, Sonnleitner, Schösswendter, Dibon, Grahovac, Schaub/Jelic dk83, Schrammel, Traustason, Joelinton/Schobesberger dk62, Thurnwald/Kvilitaia dk72 na Wober.
0 comments :
Post a Comment