News
Loading...

FIFA YAIFUNGIA NIGERIA MICHUANO YA KIMATAIFA


Shirikisho la Soka la KImataifa (Fifa), imeifungia Nigeria kushiriki michuano ya kimataifa.
Fifa imeifungia Nigeria kwa muda usiojulikana kutokna na serikali kuliingilia shirikisho la soka la nchi hiyo NFA.
Maana yake Nigeria pamoja na klabu zake zote za soka Nigeria hazitashiriki michuano ya kimataifa.

Fifa imeamua kuchukua uamuzi huo baada ya serikali ya Nigeria kuusimamisha uongozi wa NFA kwa madai kwamba ulifanya madudu wakati timu ya taifa ya nchi hiyo ikishiriki Kombe la Dunia.

Lakini Fifa ikaonya kwamba si sahihi kuingilia masuala ya soka, serikali ya Nigeria haikutekeleza onyo hilo la Fifa kwa kulisikiliza na kulifanyia kazi. Mwisho shirikisho hilo limepitisha uamuzi wa kuifungia Nigeria.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments :

Post a Comment