News
Loading...

ANGALIA UCHAMBUZI BAB KUBWA WA FAINAL YA LEO



UJERUMANI

Ujerumani watakutana na Argentina kwenye mchezo wa fainali ya Kombe la Dunia 2014 hapo baadae leo kwenye dimba la Maracana, Brasilia.
MWANA SPORT LEO inakuletea
fomesheni tarajali katika mchezo huo, line-ups na maelezo mafupi ya kila mchezaji ambaye ataanza kwenye kikosi cha kwanza katika timu yake, pamoja na makocha.

Mlinda mlango: Manuel Neuer, Bayern Munich (28)


World Cup 2014: Manuel Neuer save denies French equaliser
Kombe la Dunia 2014: Manuel Neuer aliokoa mpira uliokuwa wa kusawazisha dhidi ya Ufaransa.
 Mashindano haya yamemsaidia Manuel Neuer kuonesha ubora wake na kumfanya atajwe kuwa mlinda mlango namba moja duniani. 
 Wachambuzi wa masuala ya soka wanampa heko kutoka na uwezo wake wa kupangua michomo ya hatari na uthubutu wake kutoka langoni ili kuokoa hatari. Ameokoa hatari 21 nje ya eneo lake la 18 katika mchezo dhidi ya Algeria. 
 Amepoteza michezo mitatu pekee katika michezo 51 aliyoichezea Ujerumani. 
 Je, unajua? Ni mlinda mlango wa Costa Rica Keylor Navas pekee ambaye ameweka rekodi ya kuokoa kwa 91.3% zaidi ya Neuer mwenye 85.2% kwenye Kombe la Dunia mwaka huu. 

Beki wa kulia: Philipp Lahm, Bayern Munich (30)


Phillip Lahm
 Akielezewa na kocha wa klabu Pep Guardiola kama "mchezaji mwenye akili kuwahi kumfundisha", matokeo yake yameonekana kwenye Kombe la Dunia la mwaka huu ambapoamekuwa na uwezo wa kutoka kwenye nafasi yake ya beki wa kulia hadi kucheza kwenye nafasi ya kiungo mkabaji kama ambavyo amekuwa akifanya kwenye klabu yake ya Bayern Munich pale anapohisi kuna uwezekano wa kufanya hivyo hasa wakizidiwa, lakini Ujerumani imekuwa na ngome ngumu ya ulinzi kuliko ushambuliaji tangu pale aliporejea kwenye nafasi ya full-back kwenye mchezo wa robo fainali. Mchezo wa fainali utakuwa ni mchezo wake wa 20 wa Kombe la Dunia akiwa na Ujerumani. 
 Je, wajua? Hakuna mchezaji mchezaji yeyote aliyepiga pasi fupi zaidi ya Lahm kwenye fainali hizi (450). 

Mlinzi wa kati: Jerome Boateng, Bayern Munich (25)


Jerome Boateng
 Wakati mashindano haya yanaanza, alichezeshwa kama mlinzi wa kulia lakini akahamishwa hadi mlinzi wa kati kwa sababu ya kuungana na majeruhi na Lahm akarejeshwa nyuma. Aliumia mara mbili mapema katika mashindano haya, lakini ni mmoja kati ya wachezji wanaounda kikosi cha kwanza cha Joachim Low. Alikutana na kaka yake, Kevin-Prince wa Ghana, kwenye mchezo wao wa hatua ya makundi katika fainali ya pili mfululizo. 
 Je, wajua? Ameanza kwenye kila mchezo katika michezo 11 ya mwisho ya Ujerumani kwenye Kombe la Dunia. 

Mlinzi wa kati: Mats Hummels, Borussia Dortmund (25)


Mats Hummels
 Hakuwa na uhakika wa kuanza kwenye kikosi cha kwanza akiwa kama mlinzi wa kati kabla ya kuanza kwa fainali za Kombe la Dunia, ni miongoni mwa walinzi wanaopigania namba katika kikosi cha Ujerumani, lakini akijivunia nguvu zake ambazo zinamfanya aweze kumudu nafasi hiyo. Hakika, mlinzi huyo wa Borussia Dortmund amekuwa silaha muhimu, akifunga mara mbili kwa kichwa katika michezo dhidi ya Ureno na Ufaransa. Wakati wote huu alikuwa katika vita vikali vya kuugua mafua. 
 Je, wajua? Mama yake alikuwa mwanamke wa kwanza kutangaza mpira wa miguu kwenye Televisheni ya Ujerumani. 

Beki wa kushoto: Benedikt Howedes, Schalke (26)


Benedikt Howedes
 Ni beki wa kati katika klabu yake ya Schalke, ameisaidia kwa kiasi kikubwa Ujerumani kuziba pengo la mlinzi wa kushoto. Mchezaji mwenye kila kitu katika mashindano haya, ameanza katika kila mechi kwenye fainali za Brazil ambapo kocha Low alianza na masentahafu wanne. Kabla ya Kombe la Dunia kuanza alikuwa ndani ya gari aina ya Mercedes lililopata ajali iliyomuhusiaha dereva wa F1 Nico Rosberg, lakini hakuumia. 
 Je, wajua? Howedes amezuia mara nyingi zaidi kuliko mchezaji yeyote wa Ujerumani katika fainali hizi za Kombe la Dunia (15). 

Kiungo wa kati: Sami Khedira, Real Madrid (27)


Germany celebrate their fifth goal
Aliifungia Ujerumani bao la tano katika mchezo dhidi ya wenyeji Brazil.
 Baada ya kuumia goti mwezi Novemba, ushiri wa Khedira kwenye Kombe la Dunia ulionekana kufififa. 
 Lakini yoyote ambaye alimtilia mashaka Joachim Low kuwa na imani kwamba kiungo huyo wa Real Madrid angeweza kucheza kwenye mashindano haya, lazima ataona aibu kutokana na kiwango kizuri alichokionesha kwenye mchezo dhidi ya Brazil. 
 Tangu alipoanza kuchezeshwa sambamba na Bastian Schweinsteiger, kiungo mwenza tangu fainali za mwaka 2010, katika mchezo wa robo fainali, Ujerumani imekuwa ikionekana imara zaidi na tishio. 
 Je, wajua? Khedira aliweka rekodi ya kutengeneza goli na kufunga kwenye Kombe la Dunia kwa mara ya kwanza kwenye mchezo dhidi ya Brazil. 

Kiungo wa kati: Bastian Schweinsteiger, Bayern Munich (29)


Bastian Schweinsteiger
 Baada ya majeruhi ambayo yalishuhudia yakimuweka nje kwenye klabu yake ya Bayern Munich karibu msimu mzima, aliumia goti wakati wa mazoezi ya kabla ya Kombe la Dunia wakati wapo kambini na kukaribia kuharibu maandalizi yake kwenye fainali hizi. Kocha Joachim Low alimuwacha nje kwenye kikosi kilichoanza mechi mbili za awali, lakini nahodha msaidizi wa Ujerumani alirejea dimbani kwenye mchezo dhidi ya Brazil katika nafasi yake na kufanya vizuri. 
 Je, wajua? Schweinsteiger ameichezea Ujerumani michezo 19 ya Kombe la Dunia; ni wachezaji watatu pekee wameicheza Ujerumani mechi zaidi za Kombe la Dunia (Lothar Matthaus, Miroslav Klose na Philipp Lahm). 

Kiungo mshambuliaji: Thomas Muller, Bayern Munich (24)


Thomas Muller strike puts Germany ahead
 Mdahalo unaweza kuibuka juu ya nafasi inayomfaa Muller, lakini anacheza kama namba tisa ya uongo, mshambuliaji wa kati au mshambuliaji wa pembeni, bali atafunga magoli daima. 
 Umri wake ni miaka 24 na anakaribia kutwaa kiatu cha pili cha dhahabu huku akisaidiwa na hat-trick katika mchezo wa ufunguzi wa Kundi dhidi ya Ureno. 
 Tayari ameshaweka rekodi ya kuwa mchezaji wa tatu katika historia ya Ujerumani baada ya Teofilo Cubillas na mchezaji-mwenza Miroslav Klose kufunga mabao matano au zaidi kwenye fainali mbili tofauti za Kombe la Dunia. 
 Je, wajua? Muller amefunga mabao 10 na kutengeneza sita katika michezo 12 ya Kombe la Dunia. 

Kiungo mshambuliaji: Toni Kroos, Bayern Munich (24)


Toni Kroos scores Gemany's third goal
Hujulikana kwa ukimya wake lakini mwenye kufanya mambo ya uhakika kwenye timu ya taifa ya Ujerumani na klabu yake ya Bayern Munich, uwezo wake katika mashindano haya umemfanya awe imara zaidi.
 Alifunga mara mbili dhidi ya Brazil na hayo yalikuwa magoli yake ya kwanza kwenye fainali za Kombe la Dunia na alikuwa mchezi bora katika mchezo huo. 
 Amecheza michezo yote ila dakika mbili pekee katika michezo sita ya Ujerumani na huenda akatajwa na nchi yake kuwa mchezaji bora wa mashindano. 
 Je, wajua? Kroos amegusa mpira mara nyingi zaidi ya mchezaji yeyote katika fainali hizi za Kombe la Dunia (606) ikijumuishwa na ile ya kuvutia 135 dhidi ya Algeria. 

Kiungo mshambuliaji: Mesut Ozil, Arsenal (25)


Mesut Ozil
 Mchezaji aliyeweka rekodi ya usajili wa Arsenal bado hajaonekana kuwa na mafanikio makubwa nchini Brazil, kutokana na walinzi wengi wa Ujerumani, Paul Breitner anashauri aondolewe kwenye kikosi. Alipoteza nafasi nzuri ya kuifanya Ujerumani ipate ushindi wa 8-0 dhidi ya Brazil. Aliandikakwenye ukurasa wake wa Twitter baada ya mchezo wa nusu fainali ambayo waliishinda Brazil 7-1 kusema kwamba anategemea kipigo hakijaiathiri Brazil. 
 Je, wajua? Hakuna mchezaji yeyote wa Ujerumani aliyetengeneza nafasi nyingi zaidi kwa mchezaji-mwenza katika fainali hizi zaidi ya Ozil (15). 

Mshambuliaji: Miroslav Klose, Lazio (36)


Germany's Miroslav Klose sets World Cup goals record
 Imeandikwa kwenye nyota kwamba Klose atakuwa mfungaji bora wa muda wote wa Kombe la Dunia baada ya kumzidi nyota wa Brazil Ronaldo, dhidi ya Wabrazil, nchi Brazil. 
 Alipofunga kwa ufundi katika mchezo wa nusu fainali dhidi ya wenyeji, ilimaanisha kwamba sasa ana magoli 16 ya Kombe la Dunia. 
 Anaongoza kwa ufungaji Ujerumani akiwa na magoli 71 kwenye michezo 136, ni mchezaji wa tatu kufunga katika fainali nne za Kombe la Dunia na Ujerumani haikuwahi kupoteza mchezo ambao Klose amefunga. 
 Je, wajua? Amecheza michezo 23 ya Kombe la Dunia ambayo inamfanya kuwa katika nafasi ya pili kuwa mchezaji wa muda wote aliyecheza michezo mingi ya Kombe la Dunia nyuma ya Paolo Maldini, na Lothar Matthaus waliocheza michezo 25. 

Kocha: Joachim Low (54)


Joachim Low
 Hawezi kuelezewa kama mchezaji, lakini msaidizi huyo wa zamani wa Jurgen Klinsmann amesaidia kwa kiwango kikubwa kulibadilisha soka la Ujerumani kutoka soka lisilovutia hadi kuwa soka la burudani miongoni mwa timu za taifa ulimwenguni. Hivyo, baada ya kupoteza katika nusu fainali au fainali katika fainali tatu za Kombe la Dunia, huenda presha ikaongezeka kama atarudi mikono mitupu tena. 

ARGENTINA


Argentina line-up

Mlinda mlango: Sergio Romero, Sampdoria (27)


World Cup 2014: Argentina's Sergio Romero save denies Bosnia
Nafasi ya mlinda mlango ilikuwa ni tatizo katika kikosi cha Argentina wakati wakijiandaa kwenye mashindano haya.
 Lakini baada ya yote, Romero amefanya kila aliloweza akicheza kwa mkopo kwenye klabu ya Monaco msimu uliopita. 
 Bila shaka, kipa huyo, 27 amefungwa mabao matatu katika mechi sita nchini Brazil na kuokoa mara mbili huku akiisaidia nchi yake kutinga hatua ya fainali dhidi ya Uholanzi. 
 Je, wajua? Romero ni mlinda mlango wa kwanza wa Argentina kucheza michezo minne bila kufungwa kwenye Kombe la Dunia. 

Beki wa kulia: Pablo Zabaleta, Manchester City (29)


Pablo Zabaleta
 Beki kisiki wa Manchester City alikosa fainali za Kombe la Dunia mwaka 2010 lakini amekuwa mchezaji muhimu katika safu ya ulinzi ya Argentina nchini Brazil. Zabaleta, 29 alipost picha yake baada ya mchezo wa nusu fainali akivaa wigi la blue na bendeji akizuia sehemu ambao aliumia baada ya kukumbana na Dirk Kuyt. 
 Je, wajua? Zabaleta amepiga pasi nyingi katika moja ya tatu ya fainali za Kombe la Dunia mwaka huu zaidi ya mlinzi yeyote wa Argentina (64). 

Mlinzi wa kati: Martin Demichelis, Manchester City (33)


Martin Demichelis
 Mchezaji mwingine wa Manchester City akiwa katika jezi za timu yaifa kwa ajili ya fainali ya Kombe la Dunia. Umri wake ni miaka 33 hakuwa na athari katika hatua ya makundi wala katika mchezo wa mtoano dhidi ya Switzerland. Alianza kwenye kikosi cha kwanza katika michezo miwil iliyopitasanjari na Ezequiel Garay na akaonekna kuwa na umuhimu na huenda akaanza tena kesho kwenye mchezo wa fainali dhidi ya Ujerumani. 
 Je, wajua? Demichelis alitibua mara nane kwenye mchezo dhidi ya Uholanzi, mara tano zaidi ya mchezi yeyote wa Argentina. 

Beki wa kati: Ezequiel Garay, Zenit St Petersburg (27)


Ezequiel Garay
 Alikaribia kujiunga na Manchester United msimu uliopita, Garay aliumia jicho kwenyemchezo wa nusu fainali dhidi ya Uholanzi wakati alipokuwa akijiweka sawa wakati akifunga moja ya kiatu chake mikononi. Kama Zabaleta, aliumia kichwani kwenye mchezo dhidi ya Uholanzi lakini wakati huu akikumbana na mlinzi-mwenza Ron Vlaar. 
 Je, wajua? Ameokoa kwa kichwa mara nyingi zaidi (36) kuliko mchezaji yeyote wa safu ya ulinzi ya Argentina.  

Beki wa kushoto: Marcos Rojo, Sporting Lisbon (24)


Marcos Rojo
 Mlinzi wa Sporting Lisbon amecheza chicni ya kocha Alejandro Sabella katika klabu ya Estudientes nchini Argentina. Alihusishwa na kutaka kuhamia katika klabu za Liverpool na Chelsea na alikuwa miongonimwa wafungaji nchini Brazil wakai alipofunga katika mchezo wa hatua ya makundi dhidi ya Nigeria, akiunganisha free-kick kwa goti lake. 
 Je, wajua? Rojo amekaba mara nyingi zaidi ya mlinzi yeyote wa Argentina (17), na kutengeneza nafasi nyingi zaidi kutoka nafasi ya ulinzi (7). 

Kiungo wa kati: Javier Mascherano, Barcelona (30)


Javier Mascherano
 Anatofautiana sana na Lionel Messi lakini nakubalika zaidi na timu yake, umuhimu wake ulionekana zaidi pale alipoweza kumzuia Arjen Robben ili asifunge katika mchezo wa nusu fainali ya Kombe la Dunia. Kiungo wa zamani wa Liverpool, ambaye alikuwa muhimu pia katika fainali za Kombe la Dunia mwaka 2010, ni kiungo mkabaji - licha ya kucheza nafasi ya beki katika klabu yake ya Barcelona. 
 Je, wajua? Javier Mascherano amepiga pasi za mbali 509 na amezuia mara 28. 

Kiungo wa kulia: Lucas Biglia, Lazio (28)


Lucas Biglia
 Umri wake ni miaka 28 na anakipiga katika klabu ya Lazio nchini Italia, alianza katika kila mchezo miongoni mwa michezo minne ya awali katika mashindano haya, na alitolewa katika kila mchezo na huenda akapangwa kwenye kiungo wa kulia katika mchezo wa fainali dhidi ya Ujerumai. Kiungo huyo alianza katika michezo miwili ya mwisho. 
 Je, wajua? Lucas Biglia lipiga pasi zilizokamilika kwa 90% katika mchezo dhidi ya Uholanzi, ni kiwango kikubwa kwa kiungo wa Argentina kufanya hivyo. 

Kiungo wa kushoto: Enzo Perez, Benfica (28)


Enzo Perez
 Anajulikana kama mpambanaji na mwenye bidii, kiungo wa Benfica ni mchezaji ambaye ana kila sifa na tayari anahusishwa na kutaka kuhamia Manchester United. Majeruhi ya Angel Di Maria yalimpa nafasi ya kuanza kwenye mchezo dhidi ya Uholanzi na hakumuangusha kocha wake. Alikuwa mchezaji bora wa mwaka kwenye Ligi ya Ureno msimu uliopita. 
 Je, wajua? Enzo Perez amemaliza dakika 90 mara moja katika michezo 10 aliyoichezea Argentina (v Slovenia). 

Fowadi: Gonzalo Higuain, Napoli (26)


Gonzalo Higuain blasts Argentina into lead
Jina lake la utani ni Pipita, mshambuliaji wa Napoli alifunga hat-trick pekee katika fainali za Kombe la Dunia mwaka 2010 na alikuwa nafasi ya tatu nyuma ya Messi na Luis Suarez kwa magoli wakati wa kufuzu kwa upande wa nchi za Amerika ya Kusini.
 Alitokea benchikwenye mchezo wa ufunguzi dhidi ya Bosnia-Hercegovina na akatoa pasi iliyozaa bao la ushindi kwa Messi. 
 Alifunga goli pekee kwenye ushindi wa robo fainali dhidi ya Ubelgiji. 
 Je, wajua? Higuain amefunga magoli pungufu katika fainali za mwaka huu zaidi ya zile za 2010 licha ya kucheza michezo miwili zaidi (goli moja 2014, magoli manne 2010); akipiga mashuti machache katika fainali hizi pia (mashuti 10 mwaka huu, 13 2010). 

Fowadi: Lionel Messi, Barcelona (27)


Argentina's Lionel Messi
Mchezaji bora wa mechi nne katika michezo minne ya timu yake na kufunga magoli manne pia likiwemo goli safi dhidi ya Bosnia-Hercegovina na Iran.
 Alifunga mara mbili kwenye mchezo dhidi ya Nigeria na fowadi huyo kuonesha ishara kwamba anastahili kuwa mchezaji bora wa Dunia kwa kutawala pia Kombe la Dunia. 
 Laki, Messi, 27 hakuwa muhimu sana kwenye mchezo dhidi ya Uholanzi na alitajwa kuwa huenda ndito mwisho wake. 
 Je, wajua? Lionel Messi ametengeneza nafasi 21 katika mashindano haya, zaidi ya mchezaji yeyote katika fainali hizi. 

Fowadi: Ezequiel Lavezzi, Paris St-Germain (29)


Ezequiel Lavezzi
 Alitaka kuachana na masuala ya soka ili awe fundi umeme baada ya kukataliwa na klabu ya Boca Juniors akiwa na umri wa miaka 16, Lavezzi ni mmoja kati ya wachezaji muhimu wa Argentina kwenye fainali hizi. Ana tattoo ya Diego Maradona katika paja lake la kushoto - mtu aliyemuwacha kwenye kikosi cha Argentina kilichoshiriki fainali za Kombe la Dunia mwaka 2010. Alionekana akitema maji uelekeo wa kocha wake Alejandro Sabella wakati wa mchezo dhidi ya  Nigeria. 
 Je, wajua? Lavezzi amepiga mashuti mawili pekee kwenye fainali hizi, ni chache kuliko fowadi yeyote wa Argentina. 

Kocha: Alejandro Sabella (59)


Argentina manager Alejandro Sabella nearly falls over
Aliwahi kuwa kocha wa Sheffield United na Leeds United, Sabella ameonesha mafanikio zaidi kuliko mtangulizi wake Diego Maradona.
 Anaonekana kama mwalimu wa shule lakini mzee huyo wa miaka 59 amekuwa na mafanikio nchini Brazil na anatarajia kuijenga timu iliyojaa vipaji zaidi wakiongozwa na Messi kwenye mchezo wa fainali hapobaadae leo
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments :

Post a Comment