NGASSA SIJASAINI MBEYA CITY MIMI NI MCHEZAJI HALALI WA.......
Ngassa alisema kwamba yeye kama mchezaji soka ni ajira yake na anaamini anaweza kucheza popote wakati wowote, lakini haipendezi kuandikwa mambo ambayo si ya kweli juu yake.
“Inakuwa vizuri inapoandikwa nimesaini timu, wakati nimesaini kweli. Lakini si kusema nimesaini Mbeya City wakati sijasaini. Naiheshimu Mbeya City. Ni timu nzuri na napenda kuichezea siku moja hususan kwa sababu kocha wao, (Kinnah Phiri) nimewahi kufanya naye kazi. Lakini itakuwa vizuri iandikwe nimesaini wakati nimesaini. Kwa sasa napenda ieleweke sijasaini,”alisema.
Mchezaji huyo wa zamani wa Azam, Simba na Yanga amesema tayari amekwishakamilisha kilichomrudisha nyumbani na sasa anasubiri kutumiwa tiketi arudi kazini Oman.
“Mimi nilikuja huku kwa ruhusa maalum kwa ajili ya mambo ya kifamilia. Na baada ya kukamilisha mambo yangu, nimewatumia taarifa Fanja ili wanitumie tiketi nirejee kazini, kwa hiyo ninawasubiri wao,”alisema Ngassa.
0 comments :
Post a Comment